Daniel Manduku: Aliyekuwa Mkurugenzi wa KPA akana madai ya ufisadi
Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Nchini (KPA) Daniel Manduku amekana mashtaka ya ufisadi na vile vile matumizi mabaya ya mamlaka.
Manduku alistakiwa pamoja na Juma Fadhili Chugulu ambaye ni afisa wa ujenzi KPA anayedaiwa aliidhinisha malipo kutokana na ununuzi wa bidhaa kinyume cha sheria.
Habari Nyingine: Kiungo wa kati wa Manchester United Paul Pogba apatikana na virusi vya corona
![](https://cdn.statically.io/img/cdn.tuko.co.ke/images/1120/58a2d7be638319b1.jpeg)
Manduku alikamatwa kuhusiana na sakata ya utoaji zabuni ya thamani ya KSh 224 milioni katika mamlaka hiyo bila kufuata sheria na sera zinazohitajika.
Kila mmoja wao alishtakiwa kwa kosa la matumizi mabaya ya malaka na wawili hao kwa pamoja wakashtakiwa kwa kushirikiana katika kupanga njama ya kuitapeli kampuni hiyo mamilioni ya pesa.
Habari Nyingine: Nigeria yaahirisha ufunguzi wa safari za ndege za kimataifa
Upande wa mashtaka haukupinga kuachiliwa kwao kwa dhamana lakini uliomba mahakama kuwapa dhamana sawia na pesa zilizopotea mikononi mwao.
Manduku alikamatwa Alhamisi, Agosti 28 jioni baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma Noordin Haji kutoa amri ya kutiwa kwake nguvuni.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsaApp: 073248269.
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdjbIN4g5Zmm5qmmZq5brnAp5uuo6Virq212J6irq%2BRYrqswdGunp6mqp56uK2MpKeaZZGgrq%2BtjKaYnZmZYsaiedSfoKyZlJ57qcDMpQ%3D%3D