Kijana wa miaka 16 anaswa na chupi 14 chafu za wanawake
- Mshukiwa huyo aliingia chumbani mwa mmoja wa wahasiriwa na kuiba chupi zake lakini alinaswa wakati alikuwa anajaribu kuondoka
- Alikiri kutekeleza uhalifu huo baada ya kutumwa na jamaa mmoja ambaye sasa anasakwa na maafisa wa polisi
- Mshukiwa alipatwa na chupi zingine 14 za wanawake nyumbani kwake wakati wa uchunguzi
Jamaa mmoja mwenye umri wa miaka 16, anazuiliwa na maafisa wa polisi kwa madai ya kupatwa na chupi 14 za wanawake zilizotumika.
Adeniyi Muhammed kutoka nchini Nigeria, alikamatwa Jumamosi, Agosti 22, na polisi kufuatia ripoti ya mmoja wa wahasiriwa Amudalat Opaleye.
Habari Nyingine: Dereva ashtua watu kwa vimbwanga vyake vya kujipinda kama joka mchangani
![](https://cdn.statically.io/img/cdn.tuko.co.ke/images/1120/c0b44a6d56eb184c.jpeg)
Habari Nyingine: Shamba boi mashakani kwa kutoweka na chupi za mwajiri wake wa kike
Kulingana na ripoti ya Amudalat, Adeniyi aliingia chumbani mwake mnamo Jumanne, Agosti 18, na kuiba chupi zake lakini alinaswa wakati alikuwa anajaribu kuondoka.
Mshukiwa alipatwa na chupi zingine 14 za wanawake nyumbani kwake alipokuwa akikaguliwa.
![](https://cdn.statically.io/img/cdn.tuko.co.ke/images/720/0fgjhs3gmg2km368qg.jpeg)
Habari Nyingine: Raila na Ruto waungana kukashifu 'udikteta' wa serikali na habari zingine zilizovuma
Huku akikiri kutekeleza uhalifu huo, Adeniyi alichua kwamba alitumwa na jamaa mmoja amtafutie nguo hizo za ndani ambaye sasa polisi wameanzisha uchunguzi wa kumsaka mtu huyo.
Tukio sawia na hilo lilishuhudia humu nchini katika kaunti ya Machakos, ambapo kijakazi mmoja alikiri kumuibia mwajiri wake wa kike chupi zake.
![](https://cdn.statically.io/img/cdn.tuko.co.ke/images/720/3b8744ebe5ac1243.jpeg)
Boniface Mwania ambaye anakabiliwa na tuhuma za wizi, alikiri kuiba chupi sita za mwajiri wake wa kike aliyefahamika kama Rose Mueni.
Hakimu mkaazi wa Mahakama ya Kithimani Gilbert Sikwe aliarifiwa kwamba mshukiwa alitekeleza uhalifu huo nyumbani kwa Mueni katika kijiji cha Kwakitema eneo bunge la Yatta.
Mshukiwa huyo pia aliiba nguo za ndani za mumewe Mueni na alidai kuwa aliuza nguo hizo kwa KSh 100 kila moja.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsaApp: 073248269.
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdjbIJ3gJZmoqKikaOubsPAZqSimZuWenKCjJqlmqunlnqvrYycn66omWJ%2BdXnCoZifrV2vrm7DwKeYsJmbmnupwMyl